Ushairi wa Said Ahmed Mohamed umenielimisha na kunisisimua tangu niliposoma diwani yake ‘Sikate Tamaa nikiwa shule ya upili. Nilipozidi kutafiti nilipata kwamba mashairi yake yametumika katika mitihani ya kitaifa ya Fasihi mara si haba. Nilipofanya mtihani wangu 2001, tulitahiniwa “Nimeona”, shairi linalotoka kwa diwani hii.

Sina uhakika kuhusu kipindi cha ‘copyright’ cha mashairi haya lakini nitachukua kwamba ni sawa kutumia shairi hili kuelimisha. Hapa basi, ni shairi “Si Dunia ya Kulala” kutoka kwa diwani hii.

Umelala, bado umelala, huamki kwani?
Una dhila, bado una dhila, zitatoka lini?
Pa kulala, bado pa kulala, hujapabaini
Na chakula, hata na chakula, pia wakuhini
Si dunia ya kulala.

Naujuwe, wewe naujuwe, ndiwe mdhamini
Kama siwe, wewe kama siwe, ni dhiki baini
Jipekuwe, wewe jipekuwe, muhimu yakini
Uyajuwe, wewe uyajuwe, utoke gizani
Si dunia ya kulala

Comments

Comments are closed.